ZIJUE SABABU HIZI ZINAZOFANYA WANAWAKE WAVAE NUSU UCHI

No Comments
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEilTnLv_jeqeFaykhSxrEnW7w4hg0RgcG9MD_b5WI2kjU3yK3t3eyHYZoZBZKTLSmdrhex4JtM505yE0BXty_fGQg-5Q-Mpwgmb4IdAoef41kjoOIUPPexnYLRKaoXNpXGSMaq2mokdSbE/s1600/BYLSK-NIcAE9r5Z.jpg-large-449x350.jpg
Wengi hudhani wanawake wengi wanaovaa nguo zinazoonesha
 sehemu kubwa ya mwili(nusu uchi) huwa wanajiuza.
 Ukweli ni kuwa hiyo ni sababu mojawapo. 
Wanawake wa kundi hili huvaa nguo zinazoonesha mapaja,
 kuta za matiti, mgongo au kitovu wakiamini huwavutia wanaume
 na watawatongoza na kufanya biashara yao ya ngono. 
Lakini kuna sababu KUU
 
Sababu ni kuwa wengi huwa wanavaa vijinguo hivyo ili

 kuficha udhaifu wa maumbile yao. 

-Mathalani msichana huyo yeye mwenyewe akadhani na
 kuamini kuwa ana sura mbaya, hivyo suluhu yake ya kuficha 
udhaifu huo ni kuvaa nguo zinazoacha sehemu kubwa ya mwili
 wazi ili kutoa ujumbe kuwa "japo nina sura mbaya lakini miguu,
 tumbo, au matiti yangu mazuri". Lengo ni kuonesha kuwa japo ana
 sura mbaya lakini ana sehemu nyingine nzuri na zinazovutia. 


-Au labla binti mzuri wa sura na natural color, lakini hajaolewa.
 Naye anaweza kuvaa nusu uchi ili kuleta ujumbe kuwa
 "japo sijaolewa lakini mimi ni mzuri wa sura na viungo
 vyangu vingine" ili tu kuwavutia wanaume aidha wasione 
udhaifu wake wa kutoolewa na/au atongozwe.

-Kuna kundi la mwisho wao huvaa nusu uchi kwa vile
 tu labla anaona rafiki zake wanavaa nguo fupi na wanaambizana 
wanapendeza. Mfano: binti yuko chuo na akaona wenzio wanavaa
 nguo fupi na kila mmoja wao akivaa nguo fupi anaambiwa
 "UMEPENDEZA" hakika hapo binti hujikuta anatafuta vijinguo
 vya ajabu ili afanane na wenzio "waliopendeza". 

Watu hudhani kuwa mavazi huwasilisha tabia. 
Mfano binti akivaa nusu uchi basi huwa malaya,
 ukweli ni kuwa mabinti wengi huamini kwa kuvaa nusu uchi watakuwa
 wameficha udhaifu wao na watakuwa wametoa ujumbe kuwa
 "kama sina sura nina hiki kizuri". 

Chukulia utafiti wa haraka mabinti wengi wenye makalio
 makubwa huwa na watu huamini wana sura mbaya, kwa 
kuonesha kuwa wao hawajakosa vyote huvaa suruali za
 kubana au sketi fupi ili "shughuli" ionekane nyuma.

ya wanawake wengi kuvaa nguo za nusu uchi.
 
back to top