MAMBO 6 AMBAYO WANAUME HAWAPENDI KUFANYIWA NA MADEMU ZAO

No Comments
 




Haya niliyapata kutoka kwa mshauri wa masuala ya mahusiano, ndoa na vijana
 Frederick Kyara. Hizi ni baadhi tu nakuwekea hapa japo kuna vitu pia wanawake 
hawavipendi kutoka kwa wenzi wao wanaume. Nayo ni haya hapa, ungana nam
i kujadili jambo hili ambalo kwangu nimeona ni changamoto au niseme sikujua. 


1. Wanaume hawapendi kuambiwa cha kufanya na wenzi waoMwanamke 
unapotaka mwanaume afanye jambo usimwambie alifanye bali fanya kama
 una mpa ushauri. Kwamba John hivi kwa nini tusiweke balbu hapa kwenye
 korido maana kuna giza kweli. Badala ya hivi wewe John huoni hapa kwenye 
korido kuna giza balbu imeungua mwezi sasa hujabadilisha kwa nini?
 Weka balbu bwana. Atafanya au asifanye kabisa kwa sababu umemwambia cha kufanya. 


2. Wanaume hawapendi mwenzi mwenye makelele, mlalamishiYeye ni kulalamika 
kuanzia Jumatatu hadi Jumapili. Japo wanawake nao wanasema kuna wanaume 
walalamishii balaaa. Na wenye gubu wanasusa kula mpaka kuongea wanawanunia
 wake zao mmmmh! 


3. Wanaume hawapendi mwenzi mchafu Mchafu wa mwili wake na hata 
nyumbani kwenye suala la kutunza nyumba wanayoishi. Uchafu hufanya
 mwanamke apoteze mvuto. 


4. Wanaume hawapendi mwenzi mbishi Japo na wanawake wanasema
 wanaume ndio wabishi zaidi. Utampa mwanaume ushauri lakini haufanyii 
kazi ubishi mwingi. 





5. Wanaume hawapendi kuamrishwa na mwenzi wao Mwenzi mbabe
 anaetoa amri na kumtawala hawataki. 


6. Wanaume hawapendi kuhisiwa hisiwa na kusachiwa sachiwaKumpekua 
kwenye simu, mifuko ya suruali kwamba unamulika mwizi. Hawapendi,
 tena pengine hawajafanya jambo la kuwafanya wahisiwe vibaya.
back to top