![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPO8ut3M3UhvBtmvpn-zVQG1jkbmWAbDSNVbLcZ7_QimycepMxn_7TJyE1-yTj_C_Vu2bG420Ad8sd3rGt1RivzK6IV1N49oqbJMlvEqth1y568IloHTJm8BZzxGcMmKfYzjhwWzFKutnk/s400/MKE.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5Ko9ZYox_HHGggTw7PQPrjBtn7J25u4Hik9pGdg3nepjyaSS6OFzmY93poW-0LPpHEj73xbKT7319zX7t0VQmrx19gJUF9-zoi8j6F6EkWF80L_DuVHR-ECW2OAad7mo7PuIlNzQ7XYg/s1600/1013836_447947908640287_520053380_n.jpg)
1. Mwanamke jipende mwenyewe
Mwanamke ni lazima ujipende na kujiamini na ukigundua kuwa hisia
zako zaapenzi zimejikita kwa huyo mwanaume ambaye hisia zako
zinaamini kuwa ni yule ambaye umewahi kumuwaza kuwa ungependa
kuwa nae basi usieleze kwanza uongo maana akija gundua weeeeee……noma.
Hapa niweke wazi kuwa ni muhimu mwanamke au mwanaume,
kwa pamoja tujue kuwa tofauti yetu na mbuzi siyo miguu au
manyoya bali kitu kingine kikubwa zaidi. Kitu hikikikubwa
ndicho sisi – sisi ni jinsi tunavyofikiri ambapo kwa kufikiri
kwetu tunakuwa kama tulivyo ambao ndiyo sisi wenyewe.
2. Jifunze namna ya kuzuga
Sisemi jifunze namna ya kudanganya bali ‘’kuzuga’’ naamini naeleweka
vema ambapo wanawake wengi wenye kujua kuzuga wamekwa sumaku
kubwa kwa wapenzi wao ama kwa wabnaume wanaowahitaji.
Wanawake wenye ujuzi wa kuzuga wamekuwa wakifanikiwa kuwanasa
wanaume wengi kutokana na ujuzi wa kutumia viungo vyao walivyop
[ewa na Mungu huku baadhi wakitumia macho yao kwa kuangaliana
mara kwa mara na wanaume wanaovutiwa huku baadhi wakitumia
midomo yao kuilamba kana kwamba anasawazisha mafuta katika
midomo hiyo.
Mbinu hii inawapagawisha wanaume wengi ambao hujikuta akikuuluza
jina ama moja kwa moja akakusogelea na kukusabahi na kujitambulisha
ama kuomba namba yako ya simu, si unajua utandawazi umewapotezea
wanaume wengi ujasiri wa kutongoza zaidi atakupigia simu, si mnajua
wengi tunatongozana kupitia simu…si vibaya ingawa hamu inapotea kidogo.
3. Panga ratiba ya kutoka, ‘’siyo kusaka mabuzi’’
Wanawake wengine wamekuwa wakilaumu kuwa hawatongozwi na
wanashindwa kuwadaka wanaume wanaowataka kimapenzi huku
wao wenyewe wakiwa tatizo. Wengi hushinda nyumbani kama
watoto wa Mfalme jambo ambalo wengine wamejikuta
wakizeeka na kuanza kukumbuka hata kwa kulazimisha
kuwa walau nwapate watoto.
Hali hii mwanamke utaiepuka endapo utakuwa na walau na
ratiba zako nzuri hata kama haupendi kwenda Disko au ni geti kali basi hata
week end uwe na ratiba ya kutembea ufukweni au mahala ambako unajua kuna
watu wanajichanganya kidogo majira ya jioni na ahapa sizungumzii kuwa
unaenda kutafuta soko bali kama unajiamini kuwa unamvuto naamini uchaguzi
wako utakuwa mgumu kwasababau wengi watatamani kuwa nawe, si
unaushawishi banaaaa…
4. Kosoa kwa hekima
Mbinu hii itawasaidia sana wanawake ambao wapo tayari kwenye ndoa
na mahusiano ya kawaida ambapo kuna mahala wanawake wanajisahau na
kuwatamkia wanaume wao maneno yasiyo na hekima, kwa mfano utamsikia
mwanamke anamwambia mwanaume wake kuwa ‘’wanaume wenzako
wanajenga, wewe kila siku ahadi tu’’ kauli kama hii ni kosa na kasoro kubwa.
Ukiachiliambali kwamba hiyo ni lawama, lakini kauli kama hiyo inajenga
hisia kwa mwenzako kuwa mwanamke huyu kumbe anapenda kuwa
na wanaume kama hao hivyo wanaume wengi hawapendi kushauriwa
bila hekima na kudhani kuwa wanawake hao wanaodhani wanaume
wao hao siyo wa maana hivyo mwanamke ukitumia maneno yasiyo
na hekima huwezi kuwa sumaku kwa mwanamume wako.
Kwa leo tuishie hapa wiki ijayo na kuendelea nitakuletea mfululizo
wa tofauti zetu yaani mwanamke na mwanaume na ujua kuwa
kutentewa vizuri na mpenzi wako ni haki yako au la na hapo tutaelezana
madogomadogo yafukuzayo wapenzi.