MAREHEMU TYSON ALIVYOAGWA LEADERS CLUB

No Comments
Gari lililobeba mwili wa marehemu George Tyson likiingia ndani ya Viwanja vya Leaders Club tayari kwa shughuli nzima ya kuuaga mwili wa marehemu Tyson.
Ndugu wa marehemu Tyson wakiongoza waombolezaji pamoja na watu waliobeba jeneza kwenda katika sehemu maalum iliyoandaliwa.
Mike Sangu pamoja na Bakari Makuka wakiwa wamebeba jeneza hilo pamoja na wanakamati wengine.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick akiaga mwili wa marehemu George Otieno 'Tyson' katika Viwanja vya Leaders, Dar.
Meneja wa Kampuni ya Global Publishers, Abdallah Mrisho akitoa salamu zake za mwisho kwa mwili wa marehemu.
Mwigizaji mkongwe, Ahmed Olotu 'Mzee Chilo' naye akipita kuaga mwili huo.
Muigizaji Mahsein Awadh 'Dokta Cheni' naye akiaga.
Eshe Buheti (mbele) na Fetty Zungu nao wakipita kuaga.
Muigizaji Jacob Steven 'JB' akiaga.
Mke wa muigizaji Kulwa Kikumba 'Dude' naye alikuwepo katika kuaga.
Komedian kutoka mkoani Tanga anayejulikana kwa jina la Mwened naye alishiriki tukio la kuaga mwili wa marehemu Tyson.
Muigizaji Hashim Kambi naye akiaga.
Thea akiwa anaaga mwili wa marehemu Tyson.
Ndugu wa marehemu Tyson nao wakipita kumuaga ndugu yao.
Monalisa akisaidiwa na watu baada ya kupita kuaga mwili wa marehemu mumewe.
Wafanyakazi wa TV1 ambao walikuwa wakifanya kazi na marehemu Tyson wakiwa na nyuso za huzuni wakati wa kumuaga mfanyakazi mwenzao.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick akihutubia msibani hapo huku wanahabari wakiwa bize kupiga picha.
Mtoto wa marehemu Tyson anayejulikana kwa jina la Sonia akiongea neno kuhusiana na msiba wa baba yake.
back to top