

Picha ya marehemu Rashidi John Chilwangwa (45).
Wa kwanza ni Afisa Usalama wa Taifa Mwandamizi, Silvanus Adriano Mzeru (56) aliyeuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Aprili 29, mwaka huu maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar.
Picha ya Marehemu ambaye alikuwa Afisa Usalama wa Taifa Mwandamizi, Silvanus Adriano Mzeru (56).
Gazeti hili lilifuatilia habari hiyo na kunasa madai kwamba wauaji hao walikuwa na pikipiki aina ya Boxer. Ilielezwa kuwa wadunguaji hao walimfuatilia afisa huyo tangu maeneo ya Tazara jijini Dar.Ilidaiwa kuwa, kufika eneo hilo la uwanja wa ndege, taa za kuongozea magari zilionesha ishara ya magari yanayotokea mjini yanatakiwa kusimama lakini baada ya dakika kama mbili taa hizo ziliruhusu magari kuondoka.
MKe wa Silvanus Mzeru kushoto pichani.
Ndipo ghafla watu hao waliokuwa wamejibanza sehemu walimmiminia risasi marehemu upande wa mbele wa kioo na kumfanya apoteze uelekeo na gari lake aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili T 844 CUG kwenda kuligonga kwa nyuma gari lingine lenye namba T 786 BLS.
Mama Salma Kikwete (mbele) na akina mama wengine wakiwa katika hali ya majonzi.
“Cha ajabu sasa, baada ya kufanya kitendo kile, wale watu kwanza walipiga risasi hewani ili raia wasisogelee eneo la tukio. Halafu ndani ya gari la marehemu walikuta pesa ambazo kiwango chake hakijafahamika na ‘brifkesi’ inayodaiwa ilikuwa na nyaraka mbalimbali,” kilisema chanzo.Ukiachana na mauaji ya afisa usalama huyo, mfanyakazi mwingine wa ikulu, Rashid John Chilwangwa (45) naye alikutwa na mauti baada ya kuanguka ghafla.

Mwili wa Silvanus Mzeru wakati akisindikizwa kwa safari yake ya mwisho.
Chilwangwa alifariki dunia ghafla saa 4:20, Mei Mosi, 2014 ndani ya Uwanja wa Uhuru wakati sherehe za siku ya wafanyakazi duniani zikiendelea.
Ibada ya kumuaga marehemu Silvanus Mzeru.
Waandishi wa habari walikuwepo katika eneo la tukio na kushuhudia wafanyakazi wa ikulu na wananchi wengine wakitokwa machozi mara baada ya kupokea taarifa za kifo hicho kutoka kwa wafanyakazi wa Msalaba Mwekundu waliokuwa wakijaribu kuokoa uhai wake.Baadaye ilidaiwa kuwa, marehemu alikuwa akisumbuliwa na kisukari na siku ya tukio, presha yake ilipanda.

Marehemu Chilwangwa alizikwa Ijumaa hiyohiyo, Kisarawe, Pwani huku marehemu Mzeru akizikwa Mei 3, mwaka huu kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Mungu azilaze pema peponi, roho za marehemu hao. Amina.