KhAA! Mshiriki wa Shindano la Miss Kiswahili mwaka 2009 ambaye kwa sasa yuko nchini China akijitafutia maisha, Rehema Fabian amenaswa laivu akiwa kimahaba na kibabu cha kizungu.
Akizungumza, mnyetishaji wetu ambaye naye yuko nchini humo alisema kuwa kwa sasa mrembo huyo anajiachia na babu huyo ambaye kwa kumwangalia harakaharaka anaweza kuwa sawa na mjukuu wake.
“Unajua mapenzi ya wazee ni mazuri sana, kwanza wanajua kubembeleza, isitoshe hawakupi msongo wa mawazo mara kwa mara kama yalivyo mapenzi ya vijana na ndiyo maana Rehema akaona bora ajiachie na kibabu,” alisema mtonyaji huyo.
Rehema "Miss Kiswahili" anena
“Ahaha! Mshaanza mambo yenu, niacheni jamani nile ujana,” alisema Rehema.




