NISHA AZIDI KUWASAIDIA WASIOJIWEZA

No Comments
Nisha akiwa amebeba mzigo wa mchele, pembeni ni gari likiwa na mizigo mingine.

Akiwa anagawanya kwa familia hizo.
Akikabidhi kiroba cha mchele kwa mama mwenye familia ya watoto kumi ambayo analea watoto yatima.
Nisha, wadogo zake wakiwa kwenye picha ya pamoja na mmoja wa watoto waliopata msaada.
Hapa akiwa anawasha moto.
Nisha akiwa anapanda kwenye mkokoteni unaokokotwa na ng’ombe.
Akiwa kwenye picha ya pamoja na waliofaidika na msaada wake.
STAA wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ameendelea kuwaasaidia wasiojiweza ambapo hivi karibuni ametembelea nyumba ishirini za watu ambao hawajawahi kufikiwa na misaada na wana maisha magumu kupindukia.
Nisha alitoa misaada mbalimbali vikiwemo vinywaji, unga, mafuta, sukari na mchele  katika kijiji cha Donge Zanzibar akiwa ameambatana na wadogo zake pamoja na baadhi ya watu wa timu yake ya Team Nisha.
back to top