Kumekuwa na maswali yasiyo na majibu miongoni mwa jamii
kwamba imekuaje vijana wa kiume wamekuwa ni waongo sana
hasa linapokuja swala la kuoa? Kwa kadiri siku zinavyozidi kwenda
ndivyo ambavyo idadi ya wanaume wanaoogopa kuoa inazidi
kuongezeka. Utakuta wapenzi wanaambiana kwamba wanapendana
na kuahidiana kuwa wataoana, lakini kitakachotokea baada ya hapo
ni mwanaume kuanza kupiga chenga kwa visingizio lukuki.
Kwa nini hali hiyo hutokea?
Ukweli ni kwamba hakuna jibu la moja kwa moja juu ya tatizo
Kwa nini hali hiyo hutokea?
Ukweli ni kwamba hakuna jibu la moja kwa moja juu ya tatizo
hilo, lakini yapo mambo ambayo yanaweza kutupa angalau
tafakuri. Nitajaribu kudadavua baadhi ya sababu zinazowafanya
wanaume siku hizi kukwepa kuingia katika taasisi ya ndoa:

1 Ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano: Hapa

1 Ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano: Hapa
nawazungumzia wale watoto wa kiume waliolelewa malezi ya
upande mmoja yaani walilelewa na mama peke yao. Sina maana
ya kudharau au kutweza malezi ya mama, la hasha, lakini ni
vyema mkafahamu kwamba kuwa na baba asiye na malezi
mazuri si sawa na kutokuwa na baba. Na ndio maana nikasema
ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano. Achilia mbali aina
ya malezi atakayoyapata kwa familia yawe mazuri au mabaya lakini
lazima kutakuwa na tabia za kiume zitakazoakisi malezi ya mtoto
wa kiume katika familia husika. Watoto waliolelewa na mama
peke yao kuna kitu huwa wanakosa, kwani wanakuwa hawana
mtu wa kumchukulia kama mfano kwa upande wa jinsia ya
kiume na hapo ndipo hujikuta wakijifunza wenyewe namna
ya kuongea na kutenda kama wanaume kwa sababu katika
makuzi yao hawakupata fursa ya kuwa karibu na baba zao.
Kwa kuwa siku hizi kuna kundi kubwa la kina mama ambao
wamejikuta
wakiachiwa mzigo wa malezi ya watoto, baada ya aidha
kuachwa na waume zao au kuzalishwa na
kutelekezwa (Single mothers), na hapo ndipo
tunaposhuhudia mtoto wa kiume anapokua kwa
umri na kimo huku akiwa hana mtu wa kumuangalia
kama mfano wa mume anavyotakiwa kuwa katika
familia zaidi ya kujifunza mambo hayo kupitia katika TV,
senema au miziki. Wanaume waliopitia malezi ya aina hii
huchelewa sana kuoa kwani huyaangalia maisha ya ndoa
kwa namna ya kujaribu na ndipo hapo wengi huishia kuishi
kinyumba na wanawake kwa ajili ya kutaka kujifunza
namna ya maisha ya ndoa yanavyotakiwa kuwa na ndio
sababu huchukua muda mrefu kufanya maamuzi.
Na mara nyingi huishia kubadilisha wanawake
kutokana na kutokuwa na uhakika wa kile wanachokitafuta.

2 Mgogoro wa kiuchumi: Kuna kundi kubwa la

2 Mgogoro wa kiuchumi: Kuna kundi kubwa la
vijana siku hizi hawana ajira au hawana uhakika na
kipato. Ukweli ni kwamba hakuna mwanaume
atakayependa kujiingiza kwenye ndoa wakati
hana kazi au hana uhakika na kipato chake.
Na hiyo ni kutokana na wanawake wengi siku
hizi kuonekana kujali zaidi wanaume wenye
uhakika na kipato. Hii misemo ya wanawake
ya kebehi dhidi ya wanaume wasio na ajira au kipato,
kama vile “mwanaume suruale” ina mchango mkubwa
sana katika kuwafanya wanaume kukwepa kuoa iwapo
hawana ajira au hawana uhakika na kipato chao.

3 Wanawake wengi kuwa na kiwango cha elimu ya juu:

3 Wanawake wengi kuwa na kiwango cha elimu ya juu:
Siku hizi wanawake wengi wameibuka katika kutafuta elimu ya
juu kwa juhudi kubwa. Idadi ya wanawake
wanaojiunga na vyuo vikuu ni wengi tofauti
na ilivyokuwa zamani. Na hiyo ni kutokana
na wazazi wengi kubadili mtazamo wao juu
ya mtoto wa kike. Zamani mtoto wa kike
alichukuliwa kama kitega uchumi.
Kwa maeneo ya vijijini na katika familia masikini,
watoto wa kike walikuwa wanatazamwa kama,
‘biashara ya kesho’ ambapo watauzwa kwa njia ya mahari.
Kwa hiyo thamani yao ilikuwa ni kuolewa,
ni ile ya kibidhaa na sio kibinadamu.
Lakini tofauti na zamani siku hizi hata
kule vijijini kumekuwa na mwamko
mkubwa sana wa kumsomesha mtoto
wa kike hadi elimu ya juu.
Kutokana na mwamko huo wanawake wengi
wamejikuta wakiona elimu kama kimbilio pekee
la kuepukana na mfumo dume. Mwanamke gani
atakubali kunyanyaswa na mwanaume akiwa na
elimu yake na labda pia akiwa na kazi yake yenye
mshahara na marupurupu ya kutosha, naamini
watakuwa ni wachache sana ambao hawajiamini
au waliathiriwa na malezi. Kwa upande wa wanaume
nao, wamejikuta wakiwaogopa wanawake hawa wenye
elimu ya juu kwa hofu ya kuzidiwa kipato na labda
kukosa sauti kama mwanaume na hiyo inatokana na ego tu.

4 Wanaume huwaona wanawake kama tishio

4 Wanaume huwaona wanawake kama tishio
wanapokuwa na mafanikio makubwa kifedha: Inaweza
kutokea mwanaume anaweza kuwa na uhusiano na
mwanamke ambaye labda tu nisema ni mbangaizaji.
Wakati huo anaweza kuahidi kufunga ndoa na
mwanamke huyo, lakini iwapo itatokea mwanamke
huyo akapata mafanikio kibiashara na kuinuka kifedha.
Kama mwanamke asipokuwa makini anaweza kusababisha
mwanaume huyo akaingia mitini. Sababu kubwa hapo
inaweza kuwa ni hofu ya kuogopa kuongozwa na mwanamke.
Kumbuka kwamba mfumo dume bado umetawala
vichwani mwa wanaume wengi kutokana na malezi.
Mwanaume asiyejiamini ni vigumu sana kwake kuoa
mwanamke aliyemzidi kipato. Kwa sababu akifanyiwa
jambo dogo tu, inakuwa kama ametoneshwa.
Atahisi kutaka kutawaliwa na mwanamke huyo.
Jambo ambalo wanawake wanatakiwa
kulifahamu ni kwamba kila mwanaume
anataka kutambuliwa na kuheshimiwa
kama shujaa kabla ya kumfuata msichana.
Iwapo utakuwa umesimama iwe ni kifedha au kielimu
pale unapotafuta kupata mwenza, inabidi ujishushe
sana la sivyo utadoda.


5 Wanaume wengi siku hizi wana hofu ya majukumu,
hasa ya kulea watoto: Kutokana na malezi yao au
kile wanachokijua kuhusu watoto, baadhi ya
vijana huamini kwamba, kulea watoto ni jambo gumu sana.
Lakini wengine wanaamini kwamba, hata mke anapaswa
kulelewa kama ilivyo kwa mtoto. Hivyo wanaamua kutafuta
kwanza uwezo ambao haupatikani kiurahisi. Kuna wengine,
ambao wamefundishwa au kuelekezwa na mila na desturi
zao kwamba, kabla hawajaoa, ni lazima wawe na nyumba
kwanza, tena kwao. Kwa hiyo, hawa hadi waje wapate uwezo
wa fedha wanakuwa wameshachelewa.

6 Kuna baadhi ya wanaume, maisha
bila ya ndoa wanayaona kuwa ndiyo bora
kuliko yale ya ndoa: Kuna baadhi ya
wanawake hujirahisisha sana kwa wanaume.
Siku hizi ni jambo la kawaida sana kukuta
mwanaume anaishi na mwanamke bila ndoa,
wenyewe wanaita Trial Marriage.
Na hapo ndipo unapokuta wanaume
hawaoni tena umuhimu wa kuoa.
Sasa kama mwanamke anaweza
tu kuishi na mwanaume bila ya
ndoa na mwanaume huyo akapata
huduma zote kutoka kwa mwanamke
huyo, unadhani ni kitu gani kitamvuta
kufunga ndoa. Jambo lingine ni ile dhana
kwamba maana ya ndoa ni tendo la ndoa.
Siku hizi wanaume wengi wamejikuta wakiwa hawahitaji
tena kuoa kwa sababu tendo hilo linapatikana kiurahisi
tofauti na zamani. Siku hizi ina
wezekana kabisa kumtongoza binti leo na
kupata tendo siku hiyo hiyo…..
Na hapa siwazungumzii makahaba.
Nawazungumzia mabinti zetu ambao
wengine ukiwaona ni watu wa kuheshimiwa
ukiwaangalia kwa nje lakini kwa ndani hawana
lolote, vijana wa siku hizi wenyewe huwaita maharage ya Mbeya.
Kuna sababu nyingi zinazotajwa kusababisha wanaume
siku hizi kujivuta sana katika kufanya maamuzi ya
kutafuta mwenza. Lakini hizo chache nilizozitaja
zina mchango mkubwa.